Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Marko - Marko 8

Marko 8:5-10

Help us?
Click on verse(s) to share them!
5Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Nao wakamjibu, “Saba.”
6Basi, akawaamuru watu wakae chini. Akaitwaa ile mikate saba, akamshukuru Mungu, akaimega, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu, nao wakawagawia.
7Walikuwa pia na visamaki vichache. Yesu akavibariki, akaamuru vigawiwe watu vilevile.
8Watu wakala, wakashiba. Wakaokota mabaki yaliyosalia wakajaza makapu saba.
9Nao waliokula walikuwa watu wapatao elfu nne. Yesu akawaaga,
10na mara akapanda mashua pamoja na wanafunzi wake, akaenda wilaya ya Dalmanutha.

Read Marko 8Marko 8
Compare Marko 8:5-10Marko 8:5-10