9Wanafunzi wake wakamwuliza Yesu maana ya mfano huo.
10Naye akajibu, “Ninyi mmejaliwa kujua siri za Ufalme wa Mungu, lakini hao wengine sivyo; ila hao huambiwa kwa mifano, ili wakitazama wasiweze kuona, na wakisikia wasifahamu.
11“Basi, maana ya mfano huu ni hii: mbegu ni neno la Mungu.