Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 24

Luka 24:3-9

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3Walipoingia ndani, hawakuona mwili wa Bwana Yesu.
4Walipokuwa bado wanashangaa juu ya jambo hilo, mara watu wawili waliovaa mavazi yenye kung'aa sana, wakasimama karibu nao.
5Hao wanawake wakaingiwa na hofu, wakainama chini. Ndipo wale watu wakawaambia, “Kwa nini mnamtafuta aliye hai kati ya wafu?
6Hayuko hapa; amefufuka. Kumbukeni aliyowaambieni alipokuwa kule Galilaya:
7Ni lazima Mwana wa Mtu atolewe kwa watu waovu, nao watamsulubisha, na siku ya tatu atafufuka.”
8Hapo wanawake wakayakumbuka maneno yake,
9wakarudi kutoka kaburini, wakawapa mitume wale kumi na mmoja na wengine habari za mambo hayo yote.

Read Luka 24Luka 24
Compare Luka 24:3-9Luka 24:3-9