Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Luka - Luka 1

Luka 1:61-72

Help us?
Click on verse(s) to share them!
61Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
62Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
63Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
64Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
65Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
66Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
68“Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
69Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
70kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale.
71Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,

Read Luka 1Luka 1
Compare Luka 1:61-72Luka 1:61-72