Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 18

Luka 18:31-36

Help us?
Click on verse(s) to share them!
31Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
32Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
33Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka.”
34Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
35Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
36Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, “Kuna nini?”

Read Luka 18Luka 18
Compare Luka 18:31-36Luka 18:31-36