Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Luka 18:31-36 in Swahili (individual language)

Help us?

Luka 18:31-36 in Biblia Takatifu

31 Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
32 Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
33 Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka.”
34 Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
35 Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
36 Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, “Kuna nini?”
Luka 18 in Biblia Takatifu

Luka 18:31-36 in Biblia ya Kiswahili

31 Baada ya kuwakusanya wale kumi na wawibili, akawaambia, 'Tazama, tunapanda kwenda Yerusalemu, na mambo yote ambayo yameandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Adamu yatakamilishwa.
32 Kwa maana atatiwa mikononi mwa watu wa Mataifa na atatendewa dhihaka na jeuri, na kutemewa mate.
33 Baada ya kumchapa viboko watamwua na siku ya tatu atafufuka.'
34 Hawakuelewa mambo haya, na neno hili lilikuwa limefichwa kwao, na hawakuelewa mambo yaliyosemwa.
35 Ikawa Yesu ulipokaribia Yeriko, mtu mmoja kipofu alikuwa ameketi kando ya barabara akiomba msaada,
36 aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza nini kinatokea.
Luka 18 in Biblia ya Kiswahili