Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Yohana - Yohana 7

Yohana 7:44-51

Help us?
Click on verse(s) to share them!
44Wengine kati yao wangelimkamata, lakini hakuna aliyenyoosha mikono yake juu yake.
45Ndipo wale maofisa wakarudi kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo, nao wakawaambia, “Kwa nini hamjamleta?”
46Maofisa wakajibu, “Hakuna mtu aliyewahi kuzungumza kama huyu kabla.”
47Ndipo Mafarisayo walipowajibu, “Na nyinyi pia mmepotoshwa?
48Kuna yeyote kati ya watawala anayemwamini, au yeyote wa Mafarisayo?
49Bali hawa makutano wasiojua sheria - wamelaaniwa.”
50Nikodemo akawaambia (yeye aliyemwendea Yesu zamani, akiwa mmoja wa Mafarisayo),
51“Je sheria yetu inamhukumu mtu isipokuwa amesikilizwa kwanza na kujua anachokifanya?”

Read Yohana 7Yohana 7
Compare Yohana 7:44-51Yohana 7:44-51