Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Warumi - Warumi 2

Warumi 2:13-19

Help us?
Click on verse(s) to share them!
13Mtu hafanywi kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuisikia Sheria, bali kwa kuitii Sheria.
14Mathalan: watu wa mataifa mengine hawana Sheria ya Mose; lakini kila wanapotimiza matakwa ya Sheria wakiongozwa na dhamiri zao, wao wenyewe wanakuwa kipimo cha Sheria ingawa hawaijui Sheria.
15Mwenendo wao unaonyesha kwamba matakwa ya Sheria yameandikwa mioyoni mwao. Dhamiri zao zinashuhudia pia jambo hilo, maana fikira zao mara nyingine huwashtaki, na mara nyingine huwatetea.
16Hivyo, kufuatana na hii Habari Njema ninayohubiri, ndivyo itakavyokuwa wakati Mungu atakapohukumu mambo ya siri ya binadamu kwa njia ya Yesu Kristo.
17Na wewe, je? Wewe mwenyewe unajiita Myahudi; unaitumainia Sheria na kujivunia kuwa wa Mungu;
18kwa njia ya Sheria unajua matakwa ya Mungu na unaweza kuchagua jambo jema;
19wewe unajiona kuwa kiongozi wa vipofu na mwanga kwa wale walio gizani;

Read Warumi 2Warumi 2
Compare Warumi 2:13-19Warumi 2:13-19