Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mhubiri - Mhubiri 7

Mhubiri 7:15-25

Help us?
Click on verse(s) to share them!
15Nimeona mambo mengi katika siku zangu za ubatili. Kuna watu wenye haki ambao wanaangamia licha ya kwamba wana haki, na kuna watu waovu wanaoishi maisha marefu licha ya kwamba ni waovu.
16Usiwe mwenye haki katika macho yako mwenyewe. Kwa nini kujiharibu mwenyewe?
17Usiwe mwovu sana au mpumbavu. Kwa nini ufe kabla ya wakati wako?
18Ni vyema kwamba ushike hekima hii, na kwamba usiache haki iende zake. Kwa kuwa mtu amchae Mungu atatimiza ahadi zake zote.
19Hekima ina nguvu ndani ya mwenye hekima, zaidi ya watawala kumi katika mji.
20Hakuna mtu mwenye haki juu ya nchi anayefanya mema na hatendi dhambi.
21Usisikilize kila neno linaongelewa, kwa sababu unaweza kusikia mtumishi wako anakulaani.
22Vivyo hivyo unafahamu mwenyewe ndani ya moyo wako umewalaani wengine mara kadhaa.
23Haya yote nimeyathibitisha kwa hekima. Nikasema, “nitakuwa mwenye hekima,” lakini zaidi ambavyo ningekuwa.
24Hekima i mbali na kina sana. Ni nani awezaye kuipata?
25Nikageuza moyo wangu kujifunza kuchunguza na kutafuta hekima na ufafanuzi wa ukweli, na kufahamu kwamba ubaya ni ujinga na kwamba upumbavu ni wazimu.

Read Mhubiri 7Mhubiri 7
Compare Mhubiri 7:15-25Mhubiri 7:15-25