8Hakika, ingawa hataamka ampe kwa sababu yeye ni rafiki yake, lakini, kwa sababu ya huyo mtu kuendelea kumwomba, ataamka ampe chochote anachohitaji.
9Kwa hiyo, ombeni, nanyi mtapewa, tafuteni, nanyi mtapata, bisheni nanyi mtafunguliwa.
10Maana yeyote aombaye hupewa, atafutaye hupata na abishaye hufunguliwa.
11Mtoto akimwomba baba yake samaki, je, atampa nyoka badala ya samaki?
12Na kama akimwomba yai, je, atampa ng'e?