Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Yohana - Yohana 4

Yohana 4:2-10

Help us?
Click on verse(s) to share them!
2(ingawa Yesu mwenyewe alikuwa habatizi ila wanafunzi wake),
3alitoka Judea na akaenda Galilaya.
4Hivyo ilikuwa muhimu kupitia Samaria.
5Na akafika kwenye mji wa Samaria, unaoitwa Sikari, karibu na eneo ambalo Yakobo alimpa mwanae Yusufu.
6Na kisima cha Yakobo kilikuwa hapo. Yesu alikuwa amechoka kwa ajili ya safari na akakaa karibu na kisima. Ilikuwa muda wa mchana.
7Mwanamke Msamaria alikuja kuteka maji, na Yesu akamwambia, “Nipe maji ninywe.”
8Kwa sababu wanafunzi wake walikuwa wameenda zao mjini kununua chakula.
9Yule mwanamke akamwambia, “Inakuaje wewe Myahudi, kuniomba mimi mwanamke Msamaria, kitu cha kunywa?” Kwa sababu Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.
10Yesu akamjibu, “Kama ungelijua karama ya Mungu, na yule anayekuambia 'Nipe maji,' ungelimwomba, na angelikupa maji ya uzima.”

Read Yohana 4Yohana 4
Compare Yohana 4:2-10Yohana 4:2-10