Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 21

Luka 21:17-26

Help us?
Click on verse(s) to share them!
17Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
18Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
19Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
20“Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
21Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
22Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
23Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
24Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
25“Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
26Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.

Read Luka 21Luka 21
Compare Luka 21:17-26Luka 21:17-26