Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 4

Yohana 4:45-48

Help us?
Click on verse(s) to share them!
45Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
46Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
47Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
48Yesu akamwambia, “Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!”

Read Yohana 4Yohana 4
Compare Yohana 4:45-48Yohana 4:45-48