Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Yohana 3:31-35 in Swahili (individual language)

Help us?

Yohana 3:31-35 in Biblia Takatifu

31 “Anayekuja kutoka juu ni mkuu kuliko wote; atokaye duniani ni wa dunia, na huongea mambo ya kidunia. Lakini anayekuja kutoka mbinguni ni mkuu kuliko wote.
32 Yeye husema yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna mtu anayekubali ujumbe wake.
33 Lakini mtu yeyote anayekubali ujumbe wake anathibitisha kwamba Mungu ni kweli.
34 Yule aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, maana Mungu humjalia mtu huyo Roho wake bila kipimo.
35 Baba anampenda Mwana na amemkabidhi vitu vyote.
Yohana 3 in Biblia Takatifu

Yohana 3:31-35 in Biblia ya Kiswahili

31 Yeye atokaye juu, yu juu ya yote. Yeye aliye wa ulimwengu anatoka ulimwenguni na huongea mambo ya ki ulimwengu. Yeye atokaye mbinguni yuko juu ya yote.
32 Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna apokeaye ushuhuda wake.
33 Yeye aliye pokea ushuhuda wake amehakikisha kuwa Mungu ni mkweli.
34 Kwa sababu yeye aliyetumwa na Mungu huongea maneno ya Mungu. Kwa kuwa hampi Roho kwa kipimo.
35 Baba humpenda Mwana na amempa vitu vyote mikononi mwake.
Yohana 3 in Biblia ya Kiswahili