Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Yohana 11:22-25 in Swahili (individual language)

Help us?

Yohana 11:22-25 in Biblia Takatifu

22 Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
23 Yesu akamwambia, “Kaka yako atafufuka.”
24 Martha akamjibu, “Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho.”
25 Yesu akamwambia, “Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
Yohana 11 in Biblia Takatifu

Yohana 11:22-25 in Biblia ya Kiswahili

22 Hata sasa, najua ya kuwa lolote utakaloomba kutoka kwa Mungu, atakupatia.”
23 Yesu akamwambia, kaka yako atafufuka tena.”
24 Martha akamwambia, najua kwamba atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.”
25 Yesu akamwambia, “Mimi ni ufufuo na uzima; yeye aniaminiye, ingawa atakufa, hata hivyo atakuwa anaishi;
Yohana 11 in Biblia ya Kiswahili