Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Matendo 14:22-28 in Swahili (individual language)

Help us?

Matendo 14:22-28 in Biblia Takatifu

22 Waliwaimarisha waumini wa miji hiyo na kuwatia moyo wabaki imara katika imani. Wakawaambia, “Ni lazima sisi sote tupitie katika taabu nyingi ili tuingie katika ufalme wa Mungu.”
23 Waliteua wazee katika kila kanisa kwa ajili ya waumini, na baada ya kusali na kufunga, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana ambaye walikuwa wanamwamini.
24 Baada ya kupitia katika nchi ya Pisidia, walifika Pamfulia.
25 Baada ya kuhubiri ule ujumbe huko Perga, walikwenda Atalia.
26 Kutoka huko walisafiri kwa meli wakarudi Antiokia ambako hapo awali walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi wa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameitimiza.
27 Walipofika huko Antiokia walifanya mkutano wa kanisa la mahali hapo, wakawapa taarifa juu ya mambo Mungu aliyofanya pamoja nao, na jinsi alivyowafungulia mlango watu wa mataifa mengine mlango wa kuingia katika imani.
28 Wakakaa pamoja na wale waumini kwa muda mrefu.
Matendo 14 in Biblia Takatifu

Matendo ya Mitume 14:22-28 in Biblia ya Kiswahili

22 Waliendelea kuimarisha nafsi za wanafunzi na kutiwa moyo kuendelea katika imani, akasema, “Lazima tuingie katika ufalme wa Mungu kwa kupitia mateso mengi.”
23 Walipo wateua kwa ajili yao wazee wa kila kusanyiko la waaminio, na wakiwa wameomba na kufunga, waliwakabidhi kwa Bwana, ambaye wao walimwamini.
24 Kisha walipita katika Pisidia, walifika Pamfilia.
25 Wakati walipoongea maneno katika Perga, waliteremka kwenda Atalia.
26 Kutoka huko walipanda meli hadi Antiokia ambako walikuwa wamejitoa kwa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameikamilisha.
27 Walipofika huko Antiokia, na kulikusanya kusanyiko la pamoja, wakatoa taarifa ya mambo ambayo Mungu amefanya kwao, na jinsi alivyowafungulia mlango wa imani kwa watu wa Mataifa.
28 Walikaa kwa muda mrefu na wanafunzi.
Matendo ya Mitume 14 in Biblia ya Kiswahili