Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Matendo 11:27-30 in Swahili (individual language)

Help us?

Matendo 11:27-30 in Biblia Takatifu

27 Wakati huohuo, manabii kadhaa walikuja Antiokia kutoka Yerusalemu.
28 Basi, mmoja wao aitwaye Agabo alisimama, na kwa uwezo wa Roho akabashiri kwamba kutakuwa na njaa kubwa katika nchi yote (Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa akitawala).
29 Wale wanafunzi waliamua kila mmoja kwa kadiri ya uwezo wake apeleke chochote ili kuwasaidia wale ndugu waliokuwa wanaishi Yudea.
30 Basi, wakafanya hivyo na kupeleka mchango wao kwa wazee wa kanisa kwa mikono ya Barnaba na Saulo.
Matendo 11 in Biblia Takatifu

Matendo ya Mitume 11:27-30 in Biblia ya Kiswahili

27 Na katika siku hizi manabii wakashuka kutoka Yerusalemu mpaka Antiokia.
28 Mmoja wao ni Agabo ndilo jina lake, akasimama akiashiriwa na Roho kuwa njaa kali itatokea ulimwenguni mwote. Hii ilitokea wakati wa siku za Klaudio.
29 Kwa hiyo, wanafunzi, kila mmoja alivyo fanikiwa, waliamua kupeleka misaada kwa ndugu walioko Uyahudi.
30 Walifanya hivi; Walituma pesa kwa mkono wa Barnaba na Sauli.
Matendo ya Mitume 11 in Biblia ya Kiswahili