Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 4

Luka 4:23-30

Help us?
Click on verse(s) to share them!
23Naye akawaambia, “Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako.”
24Akaendelea kusema, “Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
25Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
26Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
27Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria.”
28Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
29Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
30Lakini Yesu akapita katikati yao, akaenda zake.

Read Luka 4Luka 4
Compare Luka 4:23-30Luka 4:23-30