Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Luka - Luka 1

Luka 1:8-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
8Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
9Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
10Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
11Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
12Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
13Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
14Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
15Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.

Read Luka 1Luka 1
Compare Luka 1:8-16Luka 1:8-16