Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Luka 17:1-5 in Swahili (individual language)

Help us?

Luka 17:1-5 in Biblia Takatifu

1 Kisha, Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Haiwezekani kabisa kusitokee vikwazo vinavyosababisha dhambi; lakini ole wake mtu yule atakayevisababisha.
2 Ingekuwa afadhali kwake kufungiwa shingoni jiwe kubwa la kusagia na kutoswa baharini, kuliko kumkwaza mmoja wa wadogo hawa.
3 Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, mwonye; akitubu, msamehe.
4 Na kama akikukosea mara saba kwa siku, na kila mara akarudi kwako akisema Nimetubu, lazima umsamehe.”
5 Mitume wakamwambia Bwana, “Utuongezee imani.”
Luka 17 in Biblia Takatifu

Luka 17:1-5 in Biblia ya Kiswahili

1 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “mambo yasababishayo watu watende dhambi hayana budi kutokea, Lakini ole wake mtu anayeyasababisha!
2 Ingekua ni heri kama mtu huyo angefungiwa jiwe zito la kusagia shingoni na kutubwa baharini, kuliko kumfanya mmoja wa hawa wadogo atende dhambi.
3 Jilindeni. Kama ndugu yako akikukosea mwonye, naye akitubu msamehe.
4 Kama akikukosea mara saba kwa siku moja na mara saba kwa siku moja akaja kwako akisema, 'ninatubu,' msamehe!”
5 Mitume wake wakamwambia Bwana, “tuongezee imani yetu.”
Luka 17 in Biblia ya Kiswahili