Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 91:5-14 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 91:5-14 in Biblia ya Kiswahili

5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
Zaburi 91 in Biblia ya Kiswahili