Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 91

Zaburi 91:5-14

Help us?
Click on verse(s) to share them!
5Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
6wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
7Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
8Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
9Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
10Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
11Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
12Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
13Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
14Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.

Read Zaburi 91Zaburi 91
Compare Zaburi 91:5-14Zaburi 91:5-14