Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 73:15-28 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 73:15-28 in Biblia ya Kiswahili

15 Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
16 Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
17 Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
18 Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
19 Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
20 Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
21 Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
22 Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
23 Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
24 Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
25 Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
26 Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.
Zaburi 73 in Biblia ya Kiswahili