Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 8

Yohana 8:31-37

Help us?
Click on verse(s) to share them!
31Basi, Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkiyazingatia mafundisho yangu mtakuwa kweli wanafunzi wangu.
32Mtaujua ukweli, nao ukweli utawapeni uhuru.”
33Nao wakamjibu, “Sisi ni wazawa wa Abrahamu, na hatujapata kamwe kuwa watumwa wa mtu yeyote yule. Una maana gani unaposema: mtakuwa huru?”
34Yesu akawajibu, “Kweli nawaambieni, kila mtu anayetenda dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35Mtumwa hana makao ya kudumu nyumbani, lakini mwana anayo makao ya kudumu.
36Kama mwana akiwapeni uhuru mtakuwa huru kweli.
37Najua kwamba ninyi ni wazawa wa Abrahamu. Hata hivyo, mnataka kuniua kwa sababu hamuyakubali mafundisho yangu.

Read Yohana 8Yohana 8
Compare Yohana 8:31-37Yohana 8:31-37