Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Yohana 4:25-33 in Swahili (individual language)

Help us?

Yohana 4:25-33 in Biblia Takatifu

25 Huyo mama akamwambia, “Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu.”
26 Yesu akamwambia, “Mimi ninayesema nawe, ndiye.”
27 Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: “Unataka nini?” au, “Kwa nini unaongea na mwanamke?”
28 Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
29 “Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?”
30 Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
31 Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: “Mwalimu, ule chakula.”
32 Lakini Yesu akawaambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
33 Wanafunzi wake wakaulizana, “Je, kuna mtu aliyemletea chakula?”
Yohana 4 in Biblia Takatifu

Yohana 4:25-33 in Biblia ya Kiswahili

25 Mwanamke akamwambia, “Ninajua kuwa Masihi anakuja, (aitwaye Kristo). Huyo atakapokuja atatwambia yote.”
26 Yesu akamwambia, “Mimi unayesema nami ndiye.”
27 Wakati huo huo wanafunzi wake wakarudi. Nao walishangaa kwa nini alikuwa akizungumza na mwanamke, lakini hakuna aliyethubutu kumuuliza, “Unataka nini?” au “Kwa nini unazungumza naye.?”
28 Hivyo mwanamke akauacha mtungi wake na akaenda mjini na akawambia watu,
29 “Njooni mwone mtu aliyeniambia mambo yangu yote niliyoyatenda, je yawezekana akawa ndiye Kristo?”
30 Wakatoka mjini wakaja kwake.
31 Wakati wa mchana wanafunzi wake walimsihi wakisema, “Rabi kula chakula.”
32 lakini yeye aliwambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
33 Wanafunzi wakaambizana, hakuna aliyemletea kitu chochotekula, “Je walileta?”
Yohana 4 in Biblia ya Kiswahili