Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Yohana - Yohana 4

Yohana 4:25-33

Help us?
Click on verse(s) to share them!
25Mwanamke akamwambia, “Ninajua kuwa Masihi anakuja, (aitwaye Kristo). Huyo atakapokuja atatwambia yote.”
26Yesu akamwambia, “Mimi unayesema nami ndiye.”
27Wakati huo huo wanafunzi wake wakarudi. Nao walishangaa kwa nini alikuwa akizungumza na mwanamke, lakini hakuna aliyethubutu kumuuliza, “Unataka nini?” au “Kwa nini unazungumza naye.?”
28Hivyo mwanamke akauacha mtungi wake na akaenda mjini na akawambia watu,
29“Njooni mwone mtu aliyeniambia mambo yangu yote niliyoyatenda, je yawezekana akawa ndiye Kristo?”
30Wakatoka mjini wakaja kwake.
31Wakati wa mchana wanafunzi wake walimsihi wakisema, “Rabi kula chakula.”
32lakini yeye aliwambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
33Wanafunzi wakaambizana, hakuna aliyemletea kitu chochotekula, “Je walileta?”

Read Yohana 4Yohana 4
Compare Yohana 4:25-33Yohana 4:25-33