Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Yohana 2:2-7 in Swahili (individual language)

Help us?

Yohana 2:2-7 in Biblia Takatifu

2 naye Yesu alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
3 Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, “Hawana divai!”
4 Yesu akamjibu, “Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado.”
5 Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.”
6 Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.
7 Yesu akawaambia, “Ijazeni mitungi hiyo maji.” Nao wakaijaza mpaka juu.
Yohana 2 in Biblia Takatifu

Yohana 2:2-7 in Biblia ya Kiswahili

2 Yesu na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa katika arusi.
3 Wakati walipoishiwa na divai, mama yake Yesu akamwambia, “Hawana divai.”
4 Yesu akajibu, “Mwanamke hiyo inanihusu nini mimi? Muda wangu mimi bado haujatimia.”
5 Mama yake akawambia watumishi, “Chochote atakachowambia fanyeni.”
6 Basi kulikuwa na mitungi sita ya mawe pale iliyowekwa kwa ajili ya kunawa katika sikukuu za Wayahudi, kila moja lilikuwa na ujazo wa nzio mbili tatu.
7 Yesu akawambia, “Ijazeni maji mitungi ya mawe.” Wakajaza hadi juu.
Yohana 2 in Biblia ya Kiswahili