Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Warumi 3:11-17 in Swahili (individual language)

Help us?

Warumi 3:11-17 in Biblia Takatifu

11 Hakuna mtu anayeelewa, wala anayemtafuta Mungu.
12 Wote wamepotoka wote wamekosa; hakuna atendaye mema, hakuna hata mmoja.
13 Makoo yao ni kama kaburi wazi, ndimi zao zimejaa udanganyifu, midomoni mwao mwatoka maneno yenye sumu kama ya nyoka.
14 Vinywa vyao vimejaa laana chungu.
15 Miguu yao iko mbioni kumwaga damu,
16 popote waendapo husababisha maafa na mateso;
17 njia ya amani hawaijui.
Warumi 3 in Biblia Takatifu

Warumi 3:11-17 in Biblia ya Kiswahili

11 Hakuna mtu ambaye anaelewa. Hakuna mtu ambaye anamtafuta Mungu.
12 Wote wamegeuka. Wao kwa pamoja wamekuwa hawana maana. Hakuna atendaye mema, la, hata mmoja.
13 Makoo yao ni kaburi lililo wazi. Ndimi zao zimedanganya. Sumu ya nyoka ipo chini ya midomo yao.
14 Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.
15 Miguu yao ina mbio kumwaga damu.
16 Uharibifu na mateso yapo katika njia zao.
17 Watu hawa hawajajua njia ya amani.
Warumi 3 in Biblia ya Kiswahili