Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 3:18-26 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 3:18-26 in Biblia ya Kiswahili

18 Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomshikilia, wale wanaomshikilia wanafuraha.
19 Kwa hekima Yehova aliweka msingi wa dunia, kwa ufahamu aliziimarisha mbingu.
20 Kwa maarifa yake vina vilipasuka na mawingu kudondosha umande wake.
21 Mwanangu, zingatia hukumu ya kweli na ufahamu, na wala usiache kuvitazama.
22 Vitakuwa uzima wa nafsi yako na urembo wa hisani wa kuvaa shingoni mwako.
23 Ndipo utatembea katika njia yako kwa usalama na mguu wako hautajikwaa;
24 ulalapo hutaogopa; utakapolala, usingizi wako utakuwa mtamu.
25 Usitishwe na hofu ya ghafula au uharibifu uliosababishwa na waovu unapotokea,
26 kwa maana Yehova utakuwa upande wako na ataulinda mguu wako usinaswe kwenye mtego.
Mithali 3 in Biblia ya Kiswahili