Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 3:15-33 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 3:15-33 in Biblia ya Kiswahili

15 Hekima inathamani zaidi kuliko kito, na hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na hekima.
16 Yeye anasiku nyingi katika mkono wake wa kuume; na mkono wake wa kushoto ni utajiri na heshima.
17 Njia zake ni njia za ukarimu na mapito yake ni amani.
18 Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomshikilia, wale wanaomshikilia wanafuraha.
19 Kwa hekima Yehova aliweka msingi wa dunia, kwa ufahamu aliziimarisha mbingu.
20 Kwa maarifa yake vina vilipasuka na mawingu kudondosha umande wake.
21 Mwanangu, zingatia hukumu ya kweli na ufahamu, na wala usiache kuvitazama.
22 Vitakuwa uzima wa nafsi yako na urembo wa hisani wa kuvaa shingoni mwako.
23 Ndipo utatembea katika njia yako kwa usalama na mguu wako hautajikwaa;
24 ulalapo hutaogopa; utakapolala, usingizi wako utakuwa mtamu.
25 Usitishwe na hofu ya ghafula au uharibifu uliosababishwa na waovu unapotokea,
26 kwa maana Yehova utakuwa upande wako na ataulinda mguu wako usinaswe kwenye mtego.
27 Usizuie mema kwa wale wanaoyastahili, wakati utendaji upo ndani ya mamlaka yako.
28 Jirani yako usimwambie, “Nenda, na uje tena, na kesho nitakupa,” wakati pesa unazo.
29 Usiweke mpango wa kumdhuru jirani yako- anayeishi jirani nawe na yeye anakuamini.
30 Usishindane na mtu pasipo sababu, ikiwa hajafanya chochote kukudhuru.
31 Usimhusudu mtu jeuri au kuchagua njia zake zozote.
32 Maana mtu mjanja ni chukizo kwa Yehova, bali humleta mtu mwaminifu kwenye tumaini lake.
33 Laana ya Yehova ipo katika nyumba ya watu waovu, bali huibariki maskani ya watu wenye haki.
Mithali 3 in Biblia ya Kiswahili