Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 3

Mithali 3:15-33

Help us?
Click on verse(s) to share them!
15Hekima inathamani zaidi kuliko kito, na hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na hekima.
16Yeye anasiku nyingi katika mkono wake wa kuume; na mkono wake wa kushoto ni utajiri na heshima.
17Njia zake ni njia za ukarimu na mapito yake ni amani.
18Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomshikilia, wale wanaomshikilia wanafuraha.
19Kwa hekima Yehova aliweka msingi wa dunia, kwa ufahamu aliziimarisha mbingu.
20Kwa maarifa yake vina vilipasuka na mawingu kudondosha umande wake.
21Mwanangu, zingatia hukumu ya kweli na ufahamu, na wala usiache kuvitazama.
22Vitakuwa uzima wa nafsi yako na urembo wa hisani wa kuvaa shingoni mwako.
23Ndipo utatembea katika njia yako kwa usalama na mguu wako hautajikwaa;
24ulalapo hutaogopa; utakapolala, usingizi wako utakuwa mtamu.
25Usitishwe na hofu ya ghafula au uharibifu uliosababishwa na waovu unapotokea,
26kwa maana Yehova utakuwa upande wako na ataulinda mguu wako usinaswe kwenye mtego.
27Usizuie mema kwa wale wanaoyastahili, wakati utendaji upo ndani ya mamlaka yako.
28Jirani yako usimwambie, “Nenda, na uje tena, na kesho nitakupa,” wakati pesa unazo.
29Usiweke mpango wa kumdhuru jirani yako- anayeishi jirani nawe na yeye anakuamini.
30Usishindane na mtu pasipo sababu, ikiwa hajafanya chochote kukudhuru.
31Usimhusudu mtu jeuri au kuchagua njia zake zozote.
32Maana mtu mjanja ni chukizo kwa Yehova, bali humleta mtu mwaminifu kwenye tumaini lake.
33Laana ya Yehova ipo katika nyumba ya watu waovu, bali huibariki maskani ya watu wenye haki.

Read Mithali 3Mithali 3
Compare Mithali 3:15-33Mithali 3:15-33