Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 3:10-20 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 3:10-20 in Biblia ya Kiswahili

10 na ndipo ghala zako zitajaa na mapipa makubwa yatafurika kwa divai mpya.
11 Mwanangu, usidharau kuadibishwa na Yohova na wala usichukie karipio lake,
12 maana Yehova huwaadibisha wale wapendao, kama baba anavyoshughulika kwa mtoto wake ampendezaye.
13 Yeye apataye hekima anafuraha, naye hupata ufahamu.
14 Kwani katika hekima unapata manufaa kuliko ukibadilisha kwa fedha na faida yake inafaa zaidi kuliko dhahabu.
15 Hekima inathamani zaidi kuliko kito, na hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na hekima.
16 Yeye anasiku nyingi katika mkono wake wa kuume; na mkono wake wa kushoto ni utajiri na heshima.
17 Njia zake ni njia za ukarimu na mapito yake ni amani.
18 Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomshikilia, wale wanaomshikilia wanafuraha.
19 Kwa hekima Yehova aliweka msingi wa dunia, kwa ufahamu aliziimarisha mbingu.
20 Kwa maarifa yake vina vilipasuka na mawingu kudondosha umande wake.
Mithali 3 in Biblia ya Kiswahili