Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 3

Mithali 3:10-20

Help us?
Click on verse(s) to share them!
10na ndipo ghala zako zitajaa na mapipa makubwa yatafurika kwa divai mpya.
11Mwanangu, usidharau kuadibishwa na Yohova na wala usichukie karipio lake,
12maana Yehova huwaadibisha wale wapendao, kama baba anavyoshughulika kwa mtoto wake ampendezaye.
13Yeye apataye hekima anafuraha, naye hupata ufahamu.
14Kwani katika hekima unapata manufaa kuliko ukibadilisha kwa fedha na faida yake inafaa zaidi kuliko dhahabu.
15Hekima inathamani zaidi kuliko kito, na hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na hekima.
16Yeye anasiku nyingi katika mkono wake wa kuume; na mkono wake wa kushoto ni utajiri na heshima.
17Njia zake ni njia za ukarimu na mapito yake ni amani.
18Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomshikilia, wale wanaomshikilia wanafuraha.
19Kwa hekima Yehova aliweka msingi wa dunia, kwa ufahamu aliziimarisha mbingu.
20Kwa maarifa yake vina vilipasuka na mawingu kudondosha umande wake.

Read Mithali 3Mithali 3
Compare Mithali 3:10-20Mithali 3:10-20