Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 31:8-20 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 31:8-20 in Biblia ya Kiswahili

8 Ongea kwa ajili yao wasioweza kuongea, kwa madai ya wote wanaopotea.
9 Ongea na uhukumu kwa vipimo vya haki na utetee dai la masikini na watu wahitaji.
10 Mke hodari ni nani anaweza kumpata? Thamani yake ni zaidi kuliko vito.
11 Moyo wa mume wake humwamini, na hatakuwa masikini.
12 Humtendea mambo mema na wala si mabaya siku zote za maisha yake.
13 Huchagua sufu na kitani, na hufanya kazi yake ya mikono kwa furaha.
14 Yupo kama meli za wafanyabiashara; huleta chakula chake kutoka mbali.
15 Huamka wakati wa usiku na kuwapa chakula watu wa kaya yake, na kugawa kazi kwa watumishi wake wa kike.
16 Hulifikiria shamba na kulinunua, kwa tunda la mikono yake hupanda shamba la mizabibu.
17 Yeye mwenyewe hujivika nguvu na kuimarisha mikono yake.
18 Huangalia ni kipi kitaleta faida nzuri kwake; usiku wote taa yake haizimishwi.
19 Mikono yake huiweka kwenye mpini wa kisokotea nyuzi na hushikilia kisokotea nyuzi.
20 Mkono wake huwafikia watu masikini; mikono yake huwafikia watu wahitaji.
Mithali 31 in Biblia ya Kiswahili