Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 31

Mithali 31:8-20

Help us?
Click on verse(s) to share them!
8Ongea kwa ajili yao wasioweza kuongea, kwa madai ya wote wanaopotea.
9Ongea na uhukumu kwa vipimo vya haki na utetee dai la masikini na watu wahitaji.
10Mke hodari ni nani anaweza kumpata? Thamani yake ni zaidi kuliko vito.
11Moyo wa mume wake humwamini, na hatakuwa masikini.
12Humtendea mambo mema na wala si mabaya siku zote za maisha yake.
13Huchagua sufu na kitani, na hufanya kazi yake ya mikono kwa furaha.
14Yupo kama meli za wafanyabiashara; huleta chakula chake kutoka mbali.
15Huamka wakati wa usiku na kuwapa chakula watu wa kaya yake, na kugawa kazi kwa watumishi wake wa kike.
16Hulifikiria shamba na kulinunua, kwa tunda la mikono yake hupanda shamba la mizabibu.
17Yeye mwenyewe hujivika nguvu na kuimarisha mikono yake.
18Huangalia ni kipi kitaleta faida nzuri kwake; usiku wote taa yake haizimishwi.
19Mikono yake huiweka kwenye mpini wa kisokotea nyuzi na hushikilia kisokotea nyuzi.
20Mkono wake huwafikia watu masikini; mikono yake huwafikia watu wahitaji.

Read Mithali 31Mithali 31
Compare Mithali 31:8-20Mithali 31:8-20