Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 31:3-11 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 31:3-11 in Biblia ya Kiswahili

3 Nguvu zako usiwape wanawake; au wenye kuharibu wafalme njia zako.
4 Lemueli, kunywa divai, siyo kwa ajili ya wafalme, wala kwa watawala kuuliza, “kileo kikali kiko wapi?”
5 Kwa sababu kama watakunywa, watasahau sheria ni nini, na kupotosha haki za wote walioonewa.
6 Wape kileo kikali watu wanaopotea na mvinyo kwa wale wenye kutaabika kwa uchungu.
7 Atakunywa na kusahau umasikini wake na hataikumbuka taabu yake.
8 Ongea kwa ajili yao wasioweza kuongea, kwa madai ya wote wanaopotea.
9 Ongea na uhukumu kwa vipimo vya haki na utetee dai la masikini na watu wahitaji.
10 Mke hodari ni nani anaweza kumpata? Thamani yake ni zaidi kuliko vito.
11 Moyo wa mume wake humwamini, na hatakuwa masikini.
Mithali 31 in Biblia ya Kiswahili