Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 31

Mithali 31:3-11

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3Nguvu zako usiwape wanawake; au wenye kuharibu wafalme njia zako.
4Lemueli, kunywa divai, siyo kwa ajili ya wafalme, wala kwa watawala kuuliza, “kileo kikali kiko wapi?”
5Kwa sababu kama watakunywa, watasahau sheria ni nini, na kupotosha haki za wote walioonewa.
6Wape kileo kikali watu wanaopotea na mvinyo kwa wale wenye kutaabika kwa uchungu.
7Atakunywa na kusahau umasikini wake na hataikumbuka taabu yake.
8Ongea kwa ajili yao wasioweza kuongea, kwa madai ya wote wanaopotea.
9Ongea na uhukumu kwa vipimo vya haki na utetee dai la masikini na watu wahitaji.
10Mke hodari ni nani anaweza kumpata? Thamani yake ni zaidi kuliko vito.
11Moyo wa mume wake humwamini, na hatakuwa masikini.

Read Mithali 31Mithali 31
Compare Mithali 31:3-11Mithali 31:3-11