Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 2:2-10 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 2:2-10 in Biblia ya Kiswahili

2 usikilize hekima na utaelekeza moyo wako katika ufahamu.
3 kama utalilia ufahamu na kupaza sauti yako kwa ajili ya ufahamu,
4 kama utautafuta kama fedha na kupekua ufahamu kama unatafuta hazina iliyojificha,
5 ndipo utakapofahamu hofu ya Yehova na utapata maarifa ya Mungu.
6 Kwa kuwa Yohova hutoa hekima, katika kinywa chake hutoka maarifa na ufahamu.
7 Yeye huhifadhi sauti ya hekima kwa wale wampendezao, yeye ni ngao kwa wale waendao katika uadilifu,
8 huongoza katika njia za haki na atalinda njia ya waaminifu kwake.
9 Ndipo utakapoelewa wema, haki, usawa na kila njia njema.
10 Maana hekima itaingia moyoni mwako na maarifa yataipendeza nafsi yako.
Mithali 2 in Biblia ya Kiswahili