Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 2:10-15 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 2:10-15 in Biblia ya Kiswahili

10 Maana hekima itaingia moyoni mwako na maarifa yataipendeza nafsi yako.
11 Busara itakulinda, ufahamu utakuongoza.
12 Vitakuokoa kutoka katika njia ya uovu, kutoka kwa wale waongeao mambo potovu.
13 Ambao huziacha njia za wema na kutembea katika njia za giza.
14 Hufurahia wanapotenda maovu na hupendezwa katika upotovu.
15 Hufuata njia za udanganyifu na kwa kutumia ghilba huficha mapito yao.
Mithali 2 in Biblia ya Kiswahili