10Maana hekima itaingia moyoni mwako na maarifa yataipendeza nafsi yako.
11Busara itakulinda, ufahamu utakuongoza.
12Vitakuokoa kutoka katika njia ya uovu, kutoka kwa wale waongeao mambo potovu.
13Ambao huziacha njia za wema na kutembea katika njia za giza.
14Hufurahia wanapotenda maovu na hupendezwa katika upotovu.
15Hufuata njia za udanganyifu na kwa kutumia ghilba huficha mapito yao.