Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 24:1-12 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 24:1-12 in Biblia ya Kiswahili

1 Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
2 kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
3 Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
4 Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
5 Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
6 maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
7 Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
8 Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
9 Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
10 Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
11 Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
12 Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
Mithali 24 in Biblia ya Kiswahili