Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 24

Mithali 24:1-12

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
2kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
3Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
4Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
5Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
6maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
7Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
8Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
9Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
10Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
11Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
12Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?

Read Mithali 24Mithali 24
Compare Mithali 24:1-12Mithali 24:1-12