18 Hakika tumaini lako halitaondolewa na siku zako za hapo baadaye.
19 Sikia- wewe! - mwanangu, na uwe mwenye busara na uelekeze moyo wako katika njia.
20 Usishirikiane pamoja na walevi, au pamoja na walaji wa nyama walafi,
21 maana mlevi na mlafi wanakuwa masikini na usingizi utawavika kwa matambara.
22 Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
23 Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.
24 Baba yake mwenye haki atafurahia sana, na yule amzaaye mtoto mwenye busara atamfurahia.