Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 21:13-20 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 21:13-20 in Biblia ya Kiswahili

13 Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
14 Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
15 Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
16 Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
17 Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
18 Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
19 Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
20 Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
Mithali 21 in Biblia ya Kiswahili