Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 21

Mithali 21:13-20

Help us?
Click on verse(s) to share them!
13Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
14Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
15Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
16Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
17Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
18Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
19Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
20Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.

Read Mithali 21Mithali 21
Compare Mithali 21:13-20Mithali 21:13-20