Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mithali 20:8-13 in Swahili (individual language)

Help us?

Mithali 20:8-13 in Biblia ya Kiswahili

8 Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
9 Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
10 Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
11 Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
12 Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
13 Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
Mithali 20 in Biblia ya Kiswahili