10 Marudi ya ukatili hungojea kwa yeyote ambaye huiacha njia na yule ambaye huchukia masahihisho atakufa.
11 Kuzimu na uharibifu vipo wazi mbele za Yehova; je si zaidi sana mioyo ya wana wa wanadamu?
12 Mwenye mzaha huchukia masahihisho; hatakwenda kwa wenye hekima.
13 Moyo wenye furaha husababisha uchangamfu wa uso, bali huzuni huvunja moyo.
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha wapumbavu hujilisha kwenye upuuzi.