10Marudi ya ukatili hungojea kwa yeyote ambaye huiacha njia na yule ambaye huchukia masahihisho atakufa.
11Kuzimu na uharibifu vipo wazi mbele za Yehova; je si zaidi sana mioyo ya wana wa wanadamu?
12Mwenye mzaha huchukia masahihisho; hatakwenda kwa wenye hekima.
13Moyo wenye furaha husababisha uchangamfu wa uso, bali huzuni huvunja moyo.
14Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha wapumbavu hujilisha kwenye upuuzi.