Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mhubiri - Mhubiri 5

Mhubiri 5:12-17

Help us?
Click on verse(s) to share them!
12Usingizi wa mfanyakazi ni mtamu, kama anakula kidogo au sana, lakini utajiri wa mtu tajiri haumuruhusu yeye kulala vizuri.
13Kuna jambo baya zaidi ambalo nimeliona chini ya jua: mali iliyowekwa akiba na mwenye nayo, inamsababishia taabu mwenyewe.
14Wakati tajiri anapopoteza utajiri wake kwa bahati mbaya, mwana wake, ambaye amemzaa, habakiziwi chochote mikononi mwake.
15Kama mtu azaliwavyo uchi kutoka tumboni mwa mamaye, vivyo hivyo ataondoka katika maisha haya akiwa uchi. Hachukui chochote kutoka katika kazi yake.
16Jambo jingine baya kabisa, kama mtu alivyo kuja ni lazima aende vivyo hivyo. Hivyo ni faida gani mtu yeyote aipatayo katika kufanya kwa ajili ya upepo?
17Wakati wa siku zake anakula gizani na anafedheheshwa sana na magonjwa na hasira.

Read Mhubiri 5Mhubiri 5
Compare Mhubiri 5:12-17Mhubiri 5:12-17