Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Matendo 28:18-20 in Swahili (individual language)

Help us?

Matendo 28:18-20 in Biblia Takatifu

18 Waliponihoji na kuona kwamba sikuwa na hatia yeyote, walitaka kuniacha.
19 Lakini Wayahudi wengine walipinga jambo hilo, nami nikalazimika kukata rufani kwa Kaisari, ingawa sikuwa na chochote cha kuwashtaki wananchi wenzangu.
20 Ni kwa sababu hiyo nimeomba kuonana na kuongea nanyi, maana nimefungwa minyororo hii kwa sababu ya tumaini lile la Israeli.”
Matendo 28 in Biblia Takatifu

Matendo ya Mitume 28:18-20 in Biblia ya Kiswahili

18 Baada ya kunihoji, walitamani kuniacha huru, kwa sababu kulikuwa hakuna sababu kwangu mimi ya kustahili adhabu ya kifo.
19 Lakini wale Wayahudi walipoongea kinyume cha shauku yao, nililazimika kukata rufaa kwa Kaisaria, japokuwa haikuwa kana kwamba naleta mashtaka juu ya taifa langu.
20 Kwa sababu ya kukata kwangu rufaa, hivyo, niliomba kuwaona na kuongea nanyi. Ni kwa sababu ya kile ambacho Israel anaujasiri kwacho, nimefungwa na kifungo hiki.
Matendo ya Mitume 28 in Biblia ya Kiswahili